• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MRADI WA SHULE BORA MBIONI KUANZA UTEKELEZAJI

Posted on: September 20th, 2022


Na Byarugaba Innocent,Morogoro

Mradi wa shule Bora unaotarajiwa kuwa mwarobaini wa kuinua kiwango cha Elimu nchini uliozinduliwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza Vicky Ford Mwezi Aprili,2022 Mkoani Pwani upo  mbioni kuanza utekelezaji wake.

Hayo yameelezwa na Mratibu wa mafunzo kutoka kutoka kwenye taasisi hiyo Ndugu Raymondi Kanyambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo maafisa Mawasiliano waliopo kwenye mamlaka za Serikali za mitaa na Wizara ya Elimu,Sayansi na teknolojia na taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo zinazotekeleza mradi huo yanayoendelea Mjini Morogoro kwenye Ukumbi wa Kingsway  ili waweze kuhamasisha na kuhabarisha Umma kuhusu malengo na mafanikio ya kuanzishwa kwa mradi.

Kanyambo ameeleza malengo manne ya mradi huo kuwa ni kuimarisha ujifunzaji,ufundishaji,kutoa Elimu jumuishi na uimarishaji wa mifumo itajayowezesha kutoa Elimu stahiki kulingana na mahitaji ya wakati.

Aidha,ameongeza kuwa pamoja na kuwajengea uwezo walimu,mradi una lengo la kuona kuwa watoto wote wanaoanza Elimu ya awali wanafanikiwa kumaliza darasa la Saba na kuendelea na Elimu nyingine pasipokuwa na sababu za kimazingira isipokuwa kama watakatisha kwa sababu nyingine ikiwemo ugonjwa.

"Mradi unafanyakazi kwa karibu na Serikali hivyo utasapoti kuboresha na kuhuwisha mitaala ili iendane na wakati ikiwemo ya watu wenye ulemavu na kuimarisha mifumo ya ufundishaji kwa wadau kuanzia ngazi ya Taifa mpaka chini" amesema Kanyambo

Kwa upande upande wake mwakilishi kutoka OR-TAMISEMI Fred Kibano amewataka maafisa Mawasiliano kuendelea kufanyakazi zao kwa weledi za kutoa taarifa zao kwani kufanya hivyo ni kuwaunganisha wananchi na Serikali ambayo imekuwa ikipeleka Maendeleo mengi lakini hawahabarishwi ipasavyo

Aidha,Mkurugenzi msaidizi kutoka Idara ya Habari MAELEZO Rodney Thadeusi amewataka maafisa Habari wote kutoka kwenye Maeneo yote kuwasilisha miradi mikakati yote inayotekelezwa ili waweze kutambua na kupima  ushiriki wao ili kama Kuna maeneo hawashirikishwi waweze kuwashauri makatibu Wakuu waboreshe eneo hilo kwani wananchi wanahitaji kupata taarifa sahihi za Serikali tena kwa wakati.

Mradi huu unatekelezwa kwenye mikoa tisa nchini utagharimu GBP 80 milioni sawa na fedha za kitanzania  Bilioni 271

Wengine walioshuhudia uzinduzi kwa upande wa Tanzania ni Waziri wa Elimu,Sayansi na teknolojia Prof.Adolf Mkenda,Naibu Waziri OR-TAMISEMI Mhe.David Silinde,Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe.Abubakar Kunenge na viongozi wengine kutoa Wizara na Mikoa ya mradi

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KIBAHA TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • TANGAZO LA MNADA WA NG'OMBE KWA WAFANYA BIASHARA WA NYAMA NA NG'OMBE ,MTAA WA MTAKUJA KATA YA PANGANI, UNAOFANYIKA KILA ALHAMISI. March 13, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • MHE.NDOMBA AZINDUA GARI MPYA AINA YA LANDCRUSER ILIYONUNULIWA KWA MAPATO YA NDANI

    November 21, 2024
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa