• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Dkt.JAFO ATOA MAELEKEZO KWENYE MAJENGO YA SERIKALI

Posted on: December 14th, 2022

Na Mwandishi Maalum,Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo ameelekeza majengo yote ya Serikali yanayojengwa katika eneo la Mtumba jijini Dodoma kuwekewa mfumo wa kuvuna maji ya mvua ili kuepusha athari za kimazingira.

Ametoa maelekezo hayo alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo jipya la Ofisi ya Makamu wa Rais katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma leo Desemba 13, 2022.

Amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi huo ikiwemo utekelezaji wa maelekezo ya kuweka mifumo ya uvunaji maji ya mvua aliyotoa alipokagua ujenzi huo mwezi Juni mwaka huu.

Dkt. Jafo amesema kuwa kujengwa kwa mifumo ya kuvuna maji ya mvua kutasaidia yasiweze kutiririka ovyo na kusababisha mmomonyoko wa udongo hivyo kuharibu mazingira.

“Kwa kweli nimefarijika sana na mnavyoendelea na utekelezaji wa mradi huu wa ujenzi wa jengo la Ofisi ya Makamu wa Rais nilipofanya ziara hapa nilitoa maelekezo na nimekuta mnayatekeleza maana mmejenga tanki hili la lita laki tano litakalopokea maji ya mvua,” amesema Dkt. Jafo.

Aidha, Waziri Jafo ametoa rai kwa mkandarasi anayejenga jengo hilo kumaliza kazi zilizobakia kwa wakati ili jengo hilo liweze kukamilika ndani ya muda uliobaki.

Awali akiwasilisha taarifa ya mradi huo Mhandisi wa SUMA JKT Sajidu Bwikizo amesema ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 50 kwa mujibu wa mpango ambapo umefikia hatua ya usukaji wa nondo na umwagaji wa zege hadi sakafu (floor) ya sita.

Pia, Msimamizi wa Mradi, Meja Benedict Meena ameahidi kuyafanyia kazi maelezo ya waziri kwa kuweka mafundi wa kutosha katika kila sakafu ili kazi hiyo ifanyike na kukamilika kwa wakati.

Ikumbukwe kuwa ujenzi wa jengo hilo unasimamiwa na Mshauri elekezi Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na kutekelezwa na Mkandarasi SUMA JKT.

Matangazo

  • INEC yahimiza Wananchi mikoa 16 kujitokeza uboreshaji Daftari awamu ya pili May 14, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO YA MIAKA MITANO YA HOSPITALI YA MJI KIBAHA

    June 27, 2025
  • WANANCHI KATA YA MBWAWA NA VISIGA WAPEWA ELIMU YA BIASHARA,NA UMUHIMU WA KODI KWA MAENDELEO,

    June 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MJI KIBAHA WAKIPEWA ELIMU YA MFUMO WA USAJIRI WA MAJENGO ODK

    June 20, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI KIBAHA IMEVUNJA RASMI BARAZA LA MADIWANI JUNI 17,2025

    June 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa