• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI IMETENGA BIL. 9.9 UJENZI WA VITUO SABA VYA ZIMAMOTO NA UOKOAJI-MAJALIWA

Posted on: April 28th, 2023

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imetenga shilingi bilioni 9.93 katika bajeti ya mwaka 2023/2024 kwa ajili ya kukamilisha miradi ya ujenzi wa vituo saba vya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

Amesema kuwa vituo hivyo vitajengwa katika Mikoa ya Songwe, Simiyu, Kagera, Njombe, Manyara, Katavi na Geita.

Ametoa kauli hiyo leo Jumatano (Aprili 26, 2023) wakati akifungua vituo vya kisasa vya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji vya Nzuguni na Chamwino mkoani Dodoma ikiwa ni sehemu ya miradi inayozinduliwa katika juma la kilele cha maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Vituo hivyo vimegharimu zaidi ya shilingi bilioni 2.3.

Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa ujenzi wa vituo hivyo pamoja na upatikanaji wa vitendea kazi vya kutosha vitasaidia kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao unakuwepo.

“Kukamilika kwa miradi hii kutasaidia kusogeza huduma za zimamoto na uokoaji karibu zaidi na wananchi na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma za zimamoto na uokoaji kwa kufika eneo la tukio kwa wakati”

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa miradi mingine inayotekelezwa na Serikali ni ujenzi wa Ofisi ya Kisasa za Jeshi la Zimamoto Temeke, Dar es Salaam, vituo vya polisi vya daraja A vya Kigamboni Dar es Salaam na Wanging’ombe Mkoani Njombe.

Mingine ni Ofisi za Uhamiaji za mikoa ya Lindi na Geita na Ofisi za Makamanda wa Polisi katika Mikoa ya Kusini Unguja na Kaskazini Unguja. “Miradi hiyo yote imegharimu zaidi ya shilingi bilioni 16”.

Ameongeza kuwa, Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kutekeleza dhamira yake ya kufanya maboresho makubwa na ya kiutendaji pamoja na ujenzi wa miundombinu muhimu ya Jeshi la Zimamoto yenye lengo la kuimarisha ufanisi katika utendaji wa jeshi hilo.

Aidha, Waziri Mkuu amelitaka Jeshi hilo lisimamie vizuri matumizi ya fedha za miradi zinazotolewa na Serikali ili kuharakisha mchakato wa utekelezaji wa miradi hiyo muhimu.

“Wasimamizi wa miradi inayotekelezwa hakikisheni kuna uwiano kati ya ujenzi wa miradi na thamani halisi ya fedha inayotolewa na Serikali”.

Kwa Upande wake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni amemshukuru Rais Dkt. Samia kwa kuridhia kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya kisasa vya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini ambavyo vitasaidia kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi

“Katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya sita tunakwenda kushuhudia mapinduzi makubwa ya ununuzi wa vifaa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambapo mchakato upo katika hatua za mwisho, tutanunua hadi helikopta za kuzimia moto”

Naye,Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John William Masunga amesema Serikali imeendelea kutatua changamoto za jeshi hilo ikiwemo kununua boti za uokoaji majini, kuwezesha kupatikana kwa mkopo wa masharti nafuu wa Euro milioni 4.9 kutoka Serikali ya Austria kwa ajili ya ununuzi wa magari 12 ya kuzima moto yakiwamo magari mawili yenye ngazi kwa ajili ya majengo marefu.

Ameongeza kuwa Serikali imeliwezesha Jeshi hilo kukamilisha ujenzi wa kituo kikuu cha zimamoto na uokoaji mkoa wa Dar es Salaam katika eneo la Temeke “Serikali pia inatekeleza Mpango wa Serikali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kupata Vitendea kazi vya Dola za Kimarekani milioni 100”

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KIBAHA TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • TANGAZO LA MNADA WA NG'OMBE KWA WAFANYA BIASHARA WA NYAMA NA NG'OMBE ,MTAA WA MTAKUJA KATA YA PANGANI, UNAOFANYIKA KILA ALHAMISI. March 13, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • MHE.NDOMBA AZINDUA GARI MPYA AINA YA LANDCRUSER ILIYONUNULIWA KWA MAPATO YA NDANI

    November 21, 2024
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa