• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkurugenzi Manspaa ya Kibaha Dkt Rogers Shemwelekwa awataka Wananchi kuchangamkia fursa za kibiashara Manspaa ya Kibaha

Posted on: July 10th, 2025


Kibaha, 10 Julai 2025

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa, amekutana na wadau na wamiliki wa viwanja vilivyoko katika eneo la Mji wa Kati (Central Business District - CBD) Kibaha Mjini, katika kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya uendelezaji wa maeneo hayo.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa na kuhudhuriwa na wamiliki wa viwanja kutoka maeneo mbalimbali ya CBD, maafisa kutoka idara ya ardhi.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Shemwelekwa amesema Halmashauri ya Kibaha imepanda hadhi na kuwa Manispaa rasmi kuanzia tarehe 20 Juni 2025, hatua inayoweka msukumo mpya kwa maendeleo ya manspaa ya kibaha.


“Kupanda kwa hadhi ya Kibaha kuwa Manispaa ni fursa na wajibu mkubwa. Tunahitaji kuona mabadiliko ya kweli katika muonekano wa mji wetu , viwanja vinapaswa kuendelezwa kwa kasi, kwa mpangilio, na kwa kuzingatia sheria zote za mipango miji na ujenzi,” alisisitiza Dkt. Shemwelekwa.


Ameongeza kuwa Manispaa imewawekea wamiliki wote wa viwanja muda wa miezi sita kuanza rasmi shughuli za ujenzi katika maeneo yao, na kuonya kuwa wasiotekeleza agizo hilo watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za ardhi na mipango miji.


Aidha, Dkt. Shemwelekwa amewahimiza wamiliki wa viwanja kushirikiana na watumishi wa idara ya ardhi kwa ukaribu ili kuhakikisha wanapata taarifa sahihi na kuepuka kudanganywa na watu wasio rasmi au vishoka.


Kwa upande wao, wamiliki wa viwanja wamempongeza Mkurugenzi Kwa juhudi za kupandisha hadhi kuwa Manispaa. Mzee Mfinanga  ( Njuweni), akizungumza kwa niaba ya wadau waliokuwepo, amesema


“Tunampongeza Mkurugenzi kwa uongozi wake na dhamira ya dhati ya kuujenga mji wa Kibaha. Sisi kama wamiliki tupo tayari kushirikiana kwa vitendo ili kufanikisha malengo haya ya pamoja.”


Kikao hicho kimeelezwa kuwa sehemu ya mpango wa Manispaa wa kuimarisha Manspaa ya Kibaha kuwa kitovu cha biashara, huduma na makazi bora, sambamba na ajenda ya maendeleo ya miji ya kisasa nchini.

Matangazo

  • INEC yahimiza Wananchi mikoa 16 kujitokeza uboreshaji Daftari awamu ya pili May 14, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mkurugenzi Manspaa ya Kibaha Dkt Rogers Shemwelekwa awataka Wananchi kuchangamkia fursa za kibiashara Manspaa ya Kibaha

    July 10, 2025
  • WATENDAJI wa Kata Manspaa ya Kibaha watembelea Halmashauri ya Mji Tunduma

    July 09, 2025
  • Mh. Mchengerwa Aipongeza Sekondari ya Kibaha atoa Maagizo

    July 09, 2025
  • Mratibu wa mapato Manspaa ya Kibaha awataka watendaji kuanza utekelezaji/ ampongeza Weo misugusugu

    July 09, 2025
  • Tazama Zote

Video

Watendaji wa Kata Manspaa ya Kibaha waibua mazito mafunzo mbeya
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa