• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Manispaa ya Kibaha Yatoa Huduma za kiafya na kuhamasisha mazoezi Kwa Wananchi

Posted on: October 25th, 2025








 


Na Netho Sichali 

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imetoa huduma bure ya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali kwa wananchi zaidi ya 200 waliopo katika Halmashauri hiyo na kuhamasisha jamii kufanya mazoezi.

Baadhi ya magonjwa yaliyofanyiwa uchunguzi ni pamoja na ugonjwa wa presha,kisukari na huduma ya kuchangia damu ambapo kati ya hao Wananchi 50 waligundulika kuwa na ugonjwa wa presha na wananchi nane wamegundulika kuwa na ugonjwa wa kisukari.

Afisa afya wa mkoa wa Pwani David Vuo alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya afya yaliyofanyika Oktoba 25/2025 katika viwanja vya bwawani vilivyopo Kata ya Tumbi Manispaa ya Kibaha.


Vuo ambaye alikuwa akimwakilisha Mganga Mkuu wa mkoa wa Pwani  Kusirye Ukio amesema kuwa wiki ya afya ni nguzo ya kampeni ya afya ( Mtu ni Afya) iliyozinduliwa mwaka 2024 na Makamu wa Rais Dkt.Philip Mpango katika  hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya stendi ya zamani ya Mailimoja Manispaa ya Kibaha.

Amesema maadhimisho ya wiki ya afya ya mwaka 2025 yamekwenda sambamba na kauli mbiu ya "Kushiriki uchaguzi wa mwaka 2025 kwa amani na utulivu "ambapo ametoa wito kwa Wananchi kuhakikisha ifikapo Oktoba 29 wajitokeze kushiriki uchaguzi kwa kuwachagua viongozi wanaowataka kwa amani na utulivu.

"Oktoba 29/2025 ni siku ya uchaguzi mkuu hivyo nawasihi Wananchi wa Manispaa ya Kibaha  na Mkoa kiujumla wajitokeze kupiga kura kwa ajili ya kuwachagua viongozi wanaowataka kwa ustawi wa nchi yetu,"amesema Vuo.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kibaha Dkt .Catherine Saguti amesema kuwa kila mwaka huwa wanaadhimisha siku ya afya (Afya Day) lakini kwa mwaka huu walianza Oktoba 18 kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii.

             

Amesema moja ya shughuli hizo ni kufanya Jogging iliyowashirikisha wadau mbalimbali pamoja na kufanya usafi wa mazingira katika Mtaro wa Soko la Loliondo na kutoa huduma bure katika vituo vya kutolea huduma ya afya .

Saguti amesema kuwa Oktoba 24 walikuwa wakitoa huduma ya upimaji wa magonjwa mbalimbali katika viwanja vya bwawani Kata ya Tumbi na Oktoba 25 ndio kilele cha maadhimisho ya wiki ya afya iliyokwenda sambamba na kufanya Jogging,kukimbiza kuku na kucheza mpira wa miguu.Wafanya Jogging wa Manispaa ya Kibaha katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya afya yaliyofanyika Oktoba 25/2025.

.    Baadhi ya wadau wakiwa katika Jogging ya maadhimisho ya kilele cha wiki ya afya ( Afya Day) yaliyofanyika Oktoba 25 katika Manispaa ya Kibaha Mkoa wa Pwani

Saguti amesema kuwa pamoja na kufanya maadhimisho hayo lakini pia ameendelea kuwahamasisha Wananchi wa Manispaa hiyo wakiwemo vijana,wa kike na wakiume na wazee kuhakikisha wanashiriki uchaguzi siku ya Oktoba 29 mwaka huu.

Mwakilishi wa Vijana Wilaya ya Kibaha Mjini Joel Kituu ametumia nafasi hiyo kuwahamasisha vijana wenzake kuona umuhimu wa kujitokeza Oktoba 29 kupiga kura kuwachagua viongozi wanaowataka.

Kituu ,amesema vijana wajitokeze kupiga kura kwa amani na utulivu kwakuwa kupiga kura ni kutimiza haki yao ya msingi na kikatiba bila kusahau bima ya afya kwa wote ni msingi bora kwa huduma ya afya.

Hata hivyo,mmoja wa wananchi wa Manispaa ya Kibaha Kassim Chamiti ameishukuru idara ya afya kwa kufanya maadhimisho hayo kwakuwa yamewasaidia kupata huduma afya bure huku akisisitiza suala la kujitokeza kupiga kura siku ya Oktoba 29 mwaka huu.






Matangazo

  • Walioteuliwa kusimamia Uchaguzi Mkuu 2025 October 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Manispaa ya Kibaha Yatoa Huduma za kiafya na kuhamasisha mazoezi Kwa Wananchi

    October 25, 2025
  • Vikundi vya Jogging Manispaa ya Kibaha vyakimbia mbio fupi na kufanya usafi lengo kuhamasisha Wananchi kushiriki kikamilifu Uchaguzi Mkuu, usafi wa mazingira

    October 18, 2025
  • Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kibaha mjini awahamasisha Wananchi kupiga kura.

    October 16, 2025
  • Heri ya siku ya Nyerere

    October 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Matangazo Mubashara Hafla ya Utiaji Saini mikataba ya Soko la Mnarani na miundombinu ya Barabara
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa