• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAVAMIZI WA MAENEO KIBAHA WATAKIWA KUPISHA ZOEZI LA UPIMAJI

Posted on: September 5th, 2022


Na Byarugaba Innocent,Kibaha.


Zaidi ya wananchi 2500 huku 1611 waliovamia eneo la Mitamba kiwanja  namba 34 wanatakiwa kuondoka kwenye eneo hilo iwapo watashindwa kulipia gharama nafuu za  upangaji na upimaji kulingana na mahitaji ya Sasa.


Zoezi hilo linafanywa na Halmashauri ya Mji Kibaha yenye mamlaka kisheria baada ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuikabidhi eneo lenye Hekta 2963 lililoanza kuvamiwa na wananchi miaka 15 iliyopita na tayari kaya 1015 zimejengwa.


Kuondolewa kwao kumeibuliwa na kamati iliyoundwa na Wizara ya Ardhi ili kubaini ukweli wa nani ana haki ya kumiliki eneo hilo kati ya wananchi na Wizara ya Mifugo na Uvuvi baada ya uwepo wa mkwamo  wa Halmashauri Mji Kibaha kulipima kutoka kwa wananchi baada ya kukasimiwa na Serikali kama mamlaka ya upangaji kisheria


Hussein Sadick kando ya kuonesha vielelezo vyote vya umiliki halali Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwalipa fidia wananchi ili kulitwaa kihalali,wamewahoji wananchi 1611kati yao zaidi ya 1000 wamekiri kununua Viwanja kwenye kiwanja namba 34 kinyemela na wengine waliwasilisha nyaraka za mauziano feki zilizoandaliwa na matapeli wakiwemo viongozi wa Kuchaguliwa ngazi ya mitaa


Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe.Abubakar Kunenge amesema kipaumbele namba moja cha Serikali ya Mhe.Rais Samia ni kuwatumikia wananchi kwa kuheshimu haki na Utawala wa kisheria hivyo kwenye hili anayestahili haki atapewa na asiyestahili hatapona kwani watafikishwa mbele ya vyombo vya sheria


Aidha,Ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kibaha imeagizwa kufuta michoro na Vibali vya ujenzi vilivyokwisha tolewa kwenye eneo hilo ili kuendelea na zoezi la upangaji na upimaji kwenye Mtaa mmoja uliosalia.


Awali wakati wa mikutano ya uhamasishaji na kutafuta suluhu ya eneo hilo,Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mheshimiwa Sara Msafiri aliwaambia wavamizi hao kuwa kujenga kwenye eneo lisilo lako kisheria ni sawa na kulala nje kwani muda usiotabirika mwenye nalo anaweza kulihitaji kwa matumizi mengine na kusababisha hasara kubwa kwenye familia,hivyo alitoa rai kwa wananchi kukubali kulipia gharama za kuhalalisha ukaazi wao kama zilivyowasilishwa na mamlaka ya upangaji,hata hivyo rai hiyo haikuwa na mafanikio.


Kwa Sasa Halmashauri ya Mji Kibaha inaendelea na upangaji na upimaji wa kiwanja namba 34 kwenye mitaa ya Lumumba,Kidimu na Mkombozi na baada ya kuhitimisha wavamizi hao watatakiwa kulipia shilingi 1,500 kwa kila mita ya Mraba ili kupata uhalali kwa kumiliki Ardhi kisheria

Matangazo

  • INEC yahimiza Wananchi mikoa 16 kujitokeza uboreshaji Daftari awamu ya pili May 14, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZA UPASUAJI ZAANZA HOSPITALI YA LULANZI

    May 27, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHUGUZI , Mhe. JAJI WA RUFAA JACOBS MWAMBEGELE LEO MEI 14,2025 AMETEMBELEA NA KUZUNGUMZA NA WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

    May 14, 2025
  • ZOEZI LA MABORESHO YA DAFTARI LA WAPIGA KURA KUANZA MEI 16 KIBAHA TC

    May 09, 2025
  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa