Na Byarugaba Innocent,Kibaha.
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mheshimiwa Nickson Simon leo Ijumaa 5 Mei,2023 ametembelea na kukagua miradi mitatu ya Maendeleo inayotekelezwa kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha yenye thamani ya Tsh.Bilioni 1,091,555,899.00
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mhandisi Mshamu Munde ametaja thamani ya miradi hiyo kuwa ni Barabara ya lami yenye urefu wa Mita 400 itakayogharimu kiasi cha Tsh. 456,000,000.00,Kituo cha afya Kongowe chenye thamani ya Tsh.449,999,999.00 na Majengo mawili,Jengo la utawala na Maktaba kwenye shule ya Sekondari Mwambisi yatakayogharimu Tsh.185,555,900.00
Mheshimiwa Simon aliyeongozana na kamati yake ya ulinzi na usalama amewapongeza wataalam kwa Usimamizi mzuri wa miradi kwani imeaksi thamani ya fedha.
Aidha,Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Nickson Simon amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha fedha nyingi kutekeleza miradi ambayo inakwenda kuwanufaisha wananchi wa Kibaha.
Haki Zote Zimahifadhiwa