• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KIBAHA MJI YAANZA KUTOA CHANJO YA POLIO KWA KISHINDO,SIKU YA KWANZA YAFIKIA ASILIMIA 30.3

Posted on: September 2nd, 2022


Na Byarugaba Innocent,Kibaha


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya imeanza zoezi la Kitaifa la kutoa chanjo ya matone ya kutokomeza Polio kwa watoto wote wenye umri wa chini ya miaka mitano kuanzia Septemba 1,2022 kukiwa na lengo la kuwafikia watoto 12,386,854 Kitaifa katika awamu hii ya tatu.

Aidha,Halmashauri ya Mji Kibaha ambayo imepewa dozi 40,000 inatarajia kutoa chanjo hiyo kwa watoto wasiopungua 38748 kwa awamu hii kwenye Kata 14 na Mitaa 73 inayounda Halmashauri hiyo ambapo tayari watoto 11,347 sawa na asilimia 30.3 wamepata chanjo siku ya kwanza

Awali akiwasilisha taarifa ya mikakati ya kufanikisha  zoezi  hilo kwenye kamati ya PHC,Mratibu wa chanjo Halmashauri ya Mji Kibaha Hope Rutatina amesema jumla ya timu 69 zenye wataalam watatu kila moja zimeundwa kwa ajili ya kufanikisha na kwamba zitatembea nyumba kwa nyumba ili kuwafikia walengwa.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri Dkt.Tulitwen Mwinuka ametoa rai kwa wazazi na walezi wote kuhamasika na kuchangamkia fursa hiyo inayotolewa bure ili kuepuka gharama kubwa za kumtibia mgonjwa wa polio kwani madhara yake ni Makubwa.

"Ndugu wajumbe wa PHC niwaombe tushirikiane kuwahamasisha wananchi kutoa ushirikiano kwa watoa huduma ya chanjo,chanjo hii ni salama na imegharamiwa na Serikali.Tuwape Elimu kuwa madhara ya ugonjwa wa Polio ni Makubwa ikiwa ni pamoja na ulemavu wa viungo ambavyo matibabu yake yanahitaji fedha nyingi.Chanjo zipo nyingi na mara zote zimekuwa na mafanikio ya kuzuia maradhi" amesema Dkt.Mwinuka

Dkt.Mwinuka ameongeza kuwa chanjo hiyo inatolewa kwa kila Mtoto mwenye umri wa chini ya miaka mitano hata kama alishawahi kupata awali kwani ugonjwa wa Polio ni hatari hivyo amewasihi Wazazi na walezi kuondoa shaka kwani iwapo Mtoto atapata madhara Serikali itagharamia matibabu yake.

Kupitia taarifa kwa Umma iliyosainiwa na Waziri wa Afya nchini Mheshimiwa Ummy Mwalimu Agosti 30,2022 imeonyesha maelekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa kila nchi kufanya kampeni ya kutoa chanjo kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano kwa awamu nne mfululizo ili aweze kupata Kinga kamili endapo kutatokea mlipuko au tishio la ugonjwa wa Polio nchini mwake.

Taarifa za kitabibu zinaonesha kuwa chanzo cha ugonjwa wa Polio husababishwa na kirusi ambacho huambukizwa kutoka kwa mtu aliyeathirika kwenda kwa mtu mwingine kwa kula au kunywa kitu kilichochafuliwa na kinyesi chenye virusi vya Polio.

Matangazo

  • INEC yahimiza Wananchi mikoa 16 kujitokeza uboreshaji Daftari awamu ya pili May 14, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZA UPASUAJI ZAANZA HOSPITALI YA LULANZI

    May 27, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHUGUZI , Mhe. JAJI WA RUFAA JACOBS MWAMBEGELE LEO MEI 14,2025 AMETEMBELEA NA KUZUNGUMZA NA WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

    May 14, 2025
  • ZOEZI LA MABORESHO YA DAFTARI LA WAPIGA KURA KUANZA MEI 16 KIBAHA TC

    May 09, 2025
  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa