• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MADIWANI KIBAHA MJINI WAPATA MBINU MPYA ZA UKUSANYAJI MAPATO

Posted on: June 24th, 2022

MADIWANI KIBAHA MJINI WAPATA MBINU MPYA ZA UKUSANYAJI MAPATO


Na Innocent Byarugaba, Kibaha


Madiwani wa halmashauri ya Mji Kibaha wamepata mafunzo ya mbinu bora za ukusanyaji wa mapato ya ndani, utekelezaji wa miradi kupitia mfumo wa  force account na maandalizi na utekelezaji wa mpango wa bajeti  katika kikaokazi cha siku moja kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo mwishoni mwa wiki kwa lengo la kuimarisha makusanyo yatakayowesha  kutoa huduma stahiki kwa wananchi na matumizi sahihi ya rasilimali fedha.


Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Kibaha Mhe.Selina Wilson Msenga amesema kuwa kuwa mafunzo hayo muhimu yametolewa wakati sahihi na kutoa rai kwa Wahe.Madiwani kuyazingatia ili yalete tija.


Aidha, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Mussa Ndomba amesema kuwa mada zote tatu ni muhimu sana ingawa zimekuwa zikitekelezwa kwa nyakati  tofauti.

“Hizi mada zimekuja kwa wakati wahe. Madiwani. Tuzisikilize kwa makini hasa ukizingatia kuwa mwaka mpya wa fedha unaoanza Julai, 2022 tutaanza kutekeleza bajeti mpya” amesema na kuongeza.


Vicent Mirambo akiwasilisha mada ya ukusanyaji wa mapato amewashauri Wahe.Madiwani kujua taratibu,vishiria na udhibiti wa mapato yanayokusanywa kwani serikali imeweka utaratibu rafiki wa kukusa nya kwa njia ya kieletroniki ili kuziba mianya ya upotevu lakini bado changamoto hiyo ipo.


Mirambo ameeleza kuwa mapato ya ndani ya halmashauri hukusanywa kutokana na makadirio yaliyowekwa na uwezo wa vyanzo vilivyopo ingawa mara nyingine makadirio huwa madogo ambayo hupelekea  makusanyo kuwa makubwa.

“Wahe. Madiwani kukusanya sana ni vizuri, lakini sio sifa njema kwani hicho ni kiashiria kuwa makadirio yenu mlipanga kidogo” amesema


Aidha ameshauri kuwa na upangaji na makadirio mazuri yatakayowezesha kutekeleza vipaumbele vilivyopo ambapo takwimu za vyanzo husika ni muhimu kuwepo ili kufanya makusanyo kuwa halisia


Hali kadhalika amewakumbusha kuwa uandaaji wa makadirio ya mapato ya ndani katika halmashauri hufanyika kwa kuzingatia Sheria, Kanuni  na miongozo ya serikali huku akikumbusha baadhi ya sheria zinazoongoza kuwa ni Sheria ya fedha za Mamlaka ya Serikali za Mitaa sura 290 (1982) na mapitio ya 2019, Memoranda  ya fedha za Mamlaka za Serikali za Mitaa 2009; Sheria ya bajeti (2015), Mwongozo wa bajeti unaotolewa kila mwaka na Wizara ya Fedha na Mipango; Sheria ndogo za Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mpango mkakati wa Halmashauri na sera za Kitaifa zinazoongoza sekta mbalimbali


Mirambo ameongeza kuwa kando ya uwepo wa kanzi data ili kufikia malengo la makadirio ni vema kutambua uwezo wa kila chanzo, kutambua vyanzo vichache vinavyobeba mapato makubwa ili kuviwekea msisitizo, kuwa na mikakati sahihi ya kukusanya, kuwianisha bajeti husika na kuweka ukomo wa bajeti ingawa Wizara husika inaweza kuongeza au kupunguza kadri itakavyoona uhalisia wa vyanzo vilivyopo kabla ya kuweka kwenye mfumo.


Katika hatua nyingine ameelezea utaratibu wa kukusanya mapato kuwa ni kutambua chanzo husika, kumtambua mlipa kodi, kufanya tathmini ya kila chanzo, kutoa bili/Control namba, kulipa, kuwasilisha benki ndani ya saa 24 baada ya kukusanya, kutoa taarifa ya kimfumo, kufuatilia wadaiwa na kufanya mapitiao ya hatua zote kwa ajili ya maboresho huku akikisistiza kuwa malipo yote yanayolipwa yatolewe risiti ya kimfumo


Kwa upande mwingine  amewakumbusha washiriki kuwa, katika suala la makusanyo ya ndani msamaha wa kutokulipa mapato au faini hutolewa na Waziri mwenye dhamana ya OR-TAMISEMI pekee na sio Madiwani na kwamba wao jukumu lao kubwa ni kuhamasisha kulipa na kuhuwisha sheria ndogo pale zitakapo kuwa zimepitwa na wakati kulingana na mahitaji


Washiriki wengine waliohudhuria mafunzo hayo ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mhandisi Mshamu Munde, Mkuu wa Idara ya  utumishi na utawala Protas Dibogo, Gerald Mbosoli aliyefundisha somo la  utekelezaji wa miradi kupitia mfumo wa  force account na maandalizi na utekelezaji wa mpango wa bajeti  pamoja Katibu tawala msaidizi anayeshughulikia masuala ya Serikali za Mitaa ndugu Yona Mwakilembe.


Matangazo

  • INEC yahimiza Wananchi mikoa 16 kujitokeza uboreshaji Daftari awamu ya pili May 14, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZA UPASUAJI ZAANZA HOSPITALI YA LULANZI

    May 27, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHUGUZI , Mhe. JAJI WA RUFAA JACOBS MWAMBEGELE LEO MEI 14,2025 AMETEMBELEA NA KUZUNGUMZA NA WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

    May 14, 2025
  • ZOEZI LA MABORESHO YA DAFTARI LA WAPIGA KURA KUANZA MEI 16 KIBAHA TC

    May 09, 2025
  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa