• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MATOKEO YA SENSA YAMEONESHA TANZANIA IMEPIGA HATUA KIMAENDELEO-MAJALIWA.

Posted on: April 17th, 2023

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 imeonesha Tanzania imepiga hatua katika kuwaletea maendeleo wananchi kwenye sekta mbalimbali ikiwemo Maji, Elimu, Afya, na Mawasiliano.
Amesema hayo leo Jumamosi (Aprili 15, 2023) wakati alipozindua Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA)-Tunguu. Hafla hiyo pia imehudhuriwa na Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Seleman Abdulah.
Amesema kuwa katika Sekta ya Elimu, takwimu za Sensa zinaonesha kuwa kiwango cha jumla cha uandikishaji kwa wanafunzi ngazi ya shule za msingi kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kimefikia asilimia 95.9 Mwaka 2022 kutoka asilimia 94.6 ilivyokuwa Mwaka 2012.
“Kiwango cha kujua kusoma na kuandika kwa watu wenye umri wa miaka 5 na kuendelea kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kimeongezeka hadi asilimia 79.1 mwaka 2022 kutoka asilimia 72.0 ilivyokuwa mwaka 2012”.
Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa sekta ya maji matokeo ya Sensa yanaonesha kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kufanya vizuri kwa kuwa asilimia 99.5 ya kaya zote zina vyanzo vya maji ambapo kati ya vyanzo hivyo asilimia 67.8 ni vyanzo vilivyoboreshwa na asilimia 32.2 ni vyanzo ambavyo havijaboreshwa.
Kwa upande wa mawasiliano, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa takwimu zinaonesha kuwa asilimia 97.5 ya Vitongoji/Mitaa/Shehia vimefikiwa na mitandao ya simu. “Kiwango hiki kinafanana na hali ilivyo kwa Tanzania Bara. Wakati huohuo Tanzania Zanzibar imefanya vizuri zaidi kwa kufikia asilimia 99.0 ya shehia ambazo zimefikiwa na mitandao ya simu”.
Aidha, Waziri Mkuu amesema kuwa takwimu zinaonesha zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania wote wapo kwenye umri wa miaka 15 hadi 64.
“Hii ni ishara nzuri katika maendeleo ya nchi, kidemographia umri huu unajulikana kama umri wa kufanya kazi Kwa maneno mengine, nchi yetu ina hazina kubwa ya nguvu kazi ambayo ni moja ya kichocheo katika kujenga uchumi imara”
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametoa rai kwa wananchi kufuatilia kwa karibu taarifa za usambazaji wa matokeo haya na kuyatumia katika kufanya maamuzi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kubaini maeneo ya uwekezaji, upatikanaji wa huduma za kijamii na maeneo ya masoko kulingana na mtawanyiko wa idadi ya watu nchini.  
Naye, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Kitaifa ya Sensa ya Watu na Makazi Hemed Seleman Abdulah amesema kuwa Sensa ya mwaka 2022 ilikuwa tofauti na Sensa zote zilizopita kwani Serikali imelenga kutumia matokeo haya kuleta mafanikio na maendeleo makubwa ndani ya nchi yetu.
“Ili matokeo haya yaweze kufikiwa ni lazima takwimu hizi zitumike katika upangaji wa mipango ya maendeleo, ni imani yetu mipango yote ya maendeleo ya nchi yetu itahusisha takwimu za sensa hii ambayo imepita kila eneo la nchi yetu”
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Jenista Mhagama amesema kuwa waitaitumia ripoti hiyo kama nyenzo muhimu ya kujenga ustawi wa watu na uendelevu wa Maendeleo ya Taifa kwa ujumla.
Naye, Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Zanzibar Salum Kassim Ali amesema kuwa matumizi ya teknolojia yamesaidia kwa kiasi kikubwa kurahisisha ukusanyaji na uchakati wa taarifa zilizotokana na sensa ya watu na makazi hivyo kuwezesha kuongeza kasi ya utoaji wa matokeo ya Sensa kwa wakati.



Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KIBAHA TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • TANGAZO LA MNADA WA NG'OMBE KWA WAFANYA BIASHARA WA NYAMA NA NG'OMBE ,MTAA WA MTAKUJA KATA YA PANGANI, UNAOFANYIKA KILA ALHAMISI. March 13, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • MHE.NDOMBA AZINDUA GARI MPYA AINA YA LANDCRUSER ILIYONUNULIWA KWA MAPATO YA NDANI

    November 21, 2024
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa