• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kibaha mjini awahamasisha Wananchi kupiga kura.

Posted on: October 16th, 2025

Kibaha, Oktoba 16, 2025 — Msimamizi wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 Jimbo la Kibaha Mjini, Bi. Theresia Kyara, amewahamasisha watumishi wa umma pamoja na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la upigaji kura litakalofanyika tarehe 29 Oktoba 2025, kwa ajili ya kumchagua diwani, mbunge na Rais.


Bi. Kyara ametoa wito huo wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha katika ukumbi wa jengo la utawala, Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, ambapo amesisitiza umuhimu wa watumishi wa umma kuwa mfano wa kuigwa kwa kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo muhimu la kidemokrasia.


“Tunapowahamasisha wananchi kwenda kupiga kura, ni wajibu wetu sisi kama watumishi wa umma kuwa mstari wa mbele kuonesha mfano. Huu ni wakati wa kuamua hatma ya uongozi wa nchi yetu kwa kupiga kura kwa amani na utulivu,” alisema Bi. Kyara.


Aidha, alieleza kuwa maandalizi yote ya uchaguzi kwa ngazi ya jimbo yamekamilika, na kilichosalia ni wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi ili kutimiza haki yao ya kikatiba.


“Tunawasihi wananchi wote wa Kibaha Mjini mjitokeze kwa wingi tarehe 29 Oktoba. Maandalizi yamekamilika, tunachosubiri sasa ni siku yenyewe ya uchaguzi. Tujitokeze kwa wingi, kwa amani na utulivu, kuchagua viongozi tunaowataka kwa mujibu wa demokrasia yetu,” aliongeza.


Bi. Kyara pia amewahimiza watumishi wa Manispaa ya Kibaha kuendelea kutoa elimu kwa jamii inayowazunguka juu ya umuhimu wa kushiriki uchaguzi, ili kuhakikisha mwitikio mkubwa kutoka kwa wapiga kura wa Kibaha Mjini.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye Usajili wa waombaji nafasi ya muda usimamizi wa Uchaguzi Mkuu 2025 October 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kibaha mjini awahamasisha Wananchi kupiga kura.

    October 16, 2025
  • Heri ya siku ya Nyerere

    October 14, 2025
  • Jeshi la zimamoto na Uokoaji laadhimisha siku ya kupunguza majanga Kwa kufanya shughuli mbalimbali

    October 13, 2025
  • TSH milioni 420 ya mapato ya ndani kutengeneza Barabara za mitaa, Wananchi wapongeza

    October 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Matangazo Mubashara Hafla ya Utiaji Saini mikataba ya Soko la Mnarani na miundombinu ya Barabara
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa