• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RAIS WA TANZANIA MHE.SAMIA SULUHU HASSAN ATOA BILIONI MBILI KUJENGA KITUO CHA AFYA MBWAWA

Posted on: July 29th, 2022

Na Byarugaba Innocent, Pwani


Wananchi wa Kata ya Mbwawa, halmashauri ya Mji Kibaha wamepaza sauti kwa Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Abubakar Kunenge ya kujengewa wodi ya wazazi na kituo cha afya ili wapate staha na kustirika wakati wa kujifungua.


Kilio hicho kimetolewa kwenye  mkutano wa kutatua kero za wananchi uliofanyika kwenye eneo la zahanati kongwe ya Mbwawa na kuhudhuria na mamia ya wananchi hivi karibuni.


Fatuma Matambo amesema hali ya wananchi kwenye huduma ya uzazi hairidhishi kwani wakati mwingine huifuata Kituo cha afya Mlandizi umbali wa KM 13 hali ambayo huchangia kusababisha vifo kwa wajawazito na watoto na kutumia fursa hiyo kuomba Uboreshaji wa huduma kwani idadi ya watu inazidi kuongezeka


Aidha,Asha Matago ambaye ni ana cheti cha  ukunga wa jadi amesema kuwa wapo akina hutumia chumba kidogo kilichopo zahanati hapo lakini wanapofika wengi wenye kuhitaji huduma huwa kwenye Mazingira magumu ya kutafuta sehemu ya kuwaweka hali ambayo huwalazimu kuwapeleka vyumba vingine visivyokuwa na miundombinu ya uzazi.


Matago ameongeza kuwa wanapolazimika kuwapeleka kituo cha afya Mlandizi wengi kutokana na kuwa na uchungu tayari hujifungulia njiani ambapo kutokana na Mazingira kutokuwa rafiki hutokwa na damu nyingi,kupatwa na degedege na kupelekea vifo.


Deusi Zabloni ambaye ni Mwenyekiti wa Serikalini ya Mtaa wa Mbwawa amesema kuwa tangu Mwaka 2020 wamekuwa na nia ya kujenga wodi ya wazazi na tayari wameshakusanya tofali 6800 na wapo tayari kuchangia hata fedha ili kuokoa maisha ya wananchi wao lakini kikwako ni eneo dogo lililopo lenye Ukubwa wa ekari 6


Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe.Sara Msafiri ameungana na kilio cha wananchi cha kujengewa wodi hiyo kwani wamekuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma za kujifungua ingawa shida yao imekuwa na kutochangamka kupata eneo lenye Ukubwa unastahili ekari 15 na kuendelea kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo cha Afya badala yake wanatamani eneo la ekari Sita litumike tofauti na miongozo ya Serikali.


Akiwatoa hofu wananchi,Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe.Kunenge amewaeleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe.Samia Suluhu Hassan imeshatoa fedha kiasi cha Bilioni Mbili kwa ajili ya Ujenzi wa kituo cha afya Mbwawa lakini fedha hizo zinaweza kupelekwa kwingine kwenye uhitaji kutokana na eneo lao kuwa dogo hivyo amewapa siku nne kutafuta eneo linastahili kutokana na Vigezo vya Wizara ya afya.


"Mhe.Samia Suluhu Hassan falsafa yake ya Uongozi ni kuwatumikia wananchi, Wakati wote anafanyakazi ya kuondoa kero ili kuboresha maisha na kuleta Maendeleo ya wananchi nchini"

Aidha, Kunenge ameeleza kuwa miongoni mwa mambo anayoyapa kipaumbele Mhe.Samia ni kuwaondolea kero akina Mama hasa upande wa uzazi ili kupunguza vifo vya watoto wachanga na wajawazito kwani hii ni changamoto kubwa kwenye ubinadamu.


Hata hivyo Kunenge ameruhusu Uongozi wa Serikali ya Mtaa kwa kushirikiana na wataalam wa Halmashauri kuanza ujenzi wa chumba cha kujifungulia kwa kutumia kiasi cha fedha shilingi milioni 9 zilizopo kwenye akaunti ya Serikali ya Mtaa na halmashauri itaendelea na ukamilishaji pale itakapofikia

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KIBAHA TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • TANGAZO LA MNADA WA NG'OMBE KWA WAFANYA BIASHARA WA NYAMA NA NG'OMBE ,MTAA WA MTAKUJA KATA YA PANGANI, UNAOFANYIKA KILA ALHAMISI. March 13, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • MHE.NDOMBA AZINDUA GARI MPYA AINA YA LANDCRUSER ILIYONUNULIWA KWA MAPATO YA NDANI

    November 21, 2024
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa