• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Ugawaji wa pikipiki kwa Maofisa Elimu kata Kibaha Mji

Posted on: August 13th, 2018

HOTUBA YA MKUU WA WILAYA YA KIBAHA MHE. ASSUMPTER MSHAMA KWENYE HAFLA YA KUKABIDHI PIKIPIKI KWA MAOFISA ELIMU KATA, ILIYOFANYIKA KWENYE VIWANJA VYA MAILIMOJA,  TAREHE 13/08/2018

Ndugu;

  • Mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini,
  • Mhe. Silvestry F. Koka, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini,
  • Katibu Tawala Wilaya,
  • Mhe.Leonard S. Mlowe, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha,
  • Waheshimiwa Madiwani,
  • Mkurugenzi wa Mji,
  • Viongozi wote wa vyama vya siasa,
  • Wakuu wa idara/Vitengo,
  • Waratibu Elimu Kata,
  • Watendaji Kata,
  • Wanahabari
  • Wananchi wote
  • Mabibi na Mabwana,
  • Itifaki imezingatiwa.

Nina furaha kusimama mbele yenu nikiwa Mkuu wenu wa wilaya ya Kibaha kutoa pongezi kubwa kwa kazi mnazofanya katika kuendeleza gurudumu la maendeleo ikiwemo Elimu katika  nchi yetu ya Tanzania.

Nipende kutoa shukrani zangu za dhati kwa Raisi wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi kubwa anazozifanya kwa kuhakikisha Elimu bila malipo inafika katika maeneo yote ya Tanzania.

Ndugu wananchi; Halmashauri ya Mji Kibaha Ina jumla ya shule za Msingi 57 na Sekondari 36. Aidha shule za Msingi za Serikali 39 na 18 za binafsi. Pia shule za Sekondari za Serikali ni 13 na binafsi 23.

Uandikishaji kwa shule za awali na darasa la kwanza (STD I) umekua ukiongezeka mwaka hadi mwaka. Kwa mwaka huu 2018 idadi ya wanafunzi wa awali Imeongezeka kutoka 3127 hadi kufikia 3176 sawa na 101% na kwa darasa la kwanza imeongezeka kutoka 4734 hadi kufikia wanafunzi 5106 sawa na 116% kwa shule za serikali.

Vilevile ufaulu wa wanafunzi wa darasa la saba umekua ukiongezeka mwaka hadi mwaka, mfano mwaka 2016 wanafunzi waliosajiliwa kuingia kidato cha kwanza walikua 2271 sawa na asilimia 76.28%, na mwaka 2017 waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza walikuwa 2608 ambapo wavulana 1331 na wasichana 1277, walioripoti wavulana 1130, wasichana 1172 jumla ni 2302 ni sawa na asilimia 88, hivyo kuingia kidato cha kwanza mwaka 2018.

Ndugu wananchi; Serikali imekusudia kuleta mapinduzi ya kiuchumi ili kuikabili Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025. Sekta ya Elimuu na mafunzo kwa mujibu wa Dira ya maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025 na mpango wa muda mrefu wa maendeleo ya haraka ya rasilimali watu kwa kutayarisha idadi ya kutosha  ya Watanzania walioelimika. Hivyo basi serikali yetu ya awamu ya tano kwa usimamizi wa jemedari wetu Mh. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kupitia mradi wa LANES (Literacy Arithmetic and Numecracy Education Support) imewezeshaa kutoa mafunzo ya Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kwa walimu wa darasa la I na II ili waweze kufundisha madarasa hayo kwa umahiri, kufadhili vituo 10 vya MEMKWA katika kila Wilaya na kuwezesha mafunzo kwa kamati za shule ili ziweze kusimamia na kuendesha shughuli za kielimu kwa weledi mkubwa.

Ndugu wananchi; Kubwa zaidi ni kutoa vitendea kazi yaani pikipiki kwa Waratibu Elimu Kata ili kurahisisha usimamizi na ufuatiliaji kwa umahiri shughuli za kielimu za ujifunzaji na ufundishaji katika maeneo yao ya kazi.

Kipekee kabisa, Nimshukuru tena Mh. Raisi Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuwezesha kupatikana pikipiki hizi ambazo leo hii mimi Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, nawakabidhi ninyi waratibu elimu kata wangu wa Halmashauri ya Mji Kibaha pikipiki hizi kuwezakutekeleza majukumu yenu kwa weledi.

Nipende kuwakumbusha majukumu yenu kwa uchache ili muweze kuyatekeleza kwa ukamilifu. Majukumu hayo ni pamoja na:

  • Kuwa kiungo kati ya shule zilizo katika kata zenu na Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Mji Kibaha kupitia idara za Elimu Msingi na Sekondari.
  • Kusimamia usimamizi wa uendeshaji wa shughuli zote za kielimu katika shule za Msingi na Sekondari zilizopo katika kata zenu.
  • Kuhakikisha fedha za Serikali, michango ya kijamii, wahisani na wadau wapenda maendeleo wote, zinazopelekwa katika shule zenu zinatumika kwa kufuata kanuni na taratibu za kisheria.
  • Kuhakikisha kuanzishwa kwa miradi ya maendeleo ya shule kama vile vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo, utengenezwaji wa madawati, nyumba za walimu, maabara na mkataba, mnashirikisha nguvukazi za wananchi wa maeneo yenu ya kazi.

Ni matumaini yangu kuwa mmesoma vyema mkataba/ mikataba mliyopewa na Mkurugenzi wenu inayoelekeza juu ya matumizi sahihi ya pikipiki mtakazo kabidhiwa leo hii.

Ndugu wananchi; Kuna changamoto ambayo inalazimu leo hii nijadili kwa kina pamoja nanyi. Changamoto hiyo ni UTORO wa wanafunzi wa shule zetu unaosababisha kutofanya mitihani ya kitaifa ya Elimu ya msingi na sekondari. Changamoto hii inapelekea kushusha ufaulu kwa ufaulu kwa Wilaya yetu.

AGIZO:

Ninawaagiza wananchi wote na watendaji wote katika kila sekta, kuhakikisha kwamba watoto wote walioandikishwa katika nyanja tofautitofauti za elimu wanahudhuria shuleni na kufanya mitihani yao yote ya ndani nay a kitaifa bila kuishia njiani.

Ninawashukuru wote kwa utulivu na kunisikiliza, ahsanteni sana.

SERIKALI YA CCM HOYEEEEEEEEEEEEEEEE,

 ELIMU SAAAFIIIII, .

                                  Assumpter Mshama,

                                   MKUU WA WILAYA,

                                        KIBAHA

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KIBAHA TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • TANGAZO LA MNADA WA NG'OMBE KWA WAFANYA BIASHARA WA NYAMA NA NG'OMBE ,MTAA WA MTAKUJA KATA YA PANGANI, UNAOFANYIKA KILA ALHAMISI. March 13, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • MHE.NDOMBA AZINDUA GARI MPYA AINA YA LANDCRUSER ILIYONUNULIWA KWA MAPATO YA NDANI

    November 21, 2024
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa