• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WALIOVAMIA ENEO LA MWEKEZAJI WAMWOMBA MKURUGENZI AWASAIDIE WASIVUNJIWE

Posted on: August 29th, 2022

WALIOVAMIA ENEO LA MWEKEZAJI WAMWOMBA MKURUGENZI AWASAIDIE WASIVUNJIWE


Na Byarugaba Innocent,Kibaha


Wakazi wa mitaa ya Viziwaziwa,Mikongeni na Sagare halmashauri ya Mji Kibaha Mkoani Pwani ,wamemwomba Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kuwafikishia ombi la kupunguziwa bei ya Ardhi kutoka shilingi 15,000 kwa mita mraba anazotaka kulipwa mwekezaji kwenye eneo walilovamia hadi shilingi 2500/- kiwango wanachodai kuwa wanauwezo nacho kulipia.


Ombi hilo limetolewa Agosti 26,2022 wakati wa Mkutano baina yao na Uongozi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha uliofanyika Viziwaziwa ikiwa ni mwendelezo wa mikutano kadhaa ambayo imekuwa ikifanyika ili kutafuta suluhu ya Mgogoro wa ardhi hiyo kwa zaidi ya Miaka 10 Sasa ambapo wananchi hao wanadaiwa kuvamia na kuweka Makazi

"sisi tuliingia hapa kama mafuriko wengi tulitapeliwa kwa kuuziwa eneo hilo bila kujua.Tumeshakaa kwa miaka mingi hivyo tunakuomba Mkurugenzi tufikishie ombi letu kwa mwekezaji la kupunguziwa bei,"amesema Innocent Kimaro.


Aidha,Geoffrey Mfugale amesema kuwa ni vema mwekezaji huyo akawapunguzia kiwango cha bei kufikia 2500 kwani wakazi wengi wa mitaa hiyo vipato vyao ni duni na kwamba hawawezi kumudu gharama zinazotakiwa na mwekezaji.


Kwa upande wake Franza Teve amesema kuwa Mgogoro huo umekuwa ukiwasumbua kwa miaka mingi na wametumia gharama kubwa kutafuta suluhu na mwisho mwekezaji ameonekana ana haki hata hivyo bado wananchi wanaomba wapunguziwe,walipe ili waweze kupata uhalali  wa umiliki wa maeneo hayo ili waishi kwa amani.


Kaimu Mkuu wa Idara ya Ardhi amewaeleza wavamizi hao kuwa bei elekezi ya Ardhi kwa eneo la Viziwaziwa ni kati ya shilingi 5000-6000 ambapo Ardhi kwa matumizi ya Makazi pekee ni 5000 huku Makazi na Biashara ikiwa ni 6000.


Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha Mhandisi Mshamu Munde ameahidi kufikisha ombi lao kwa mwekezaji huku akitoa rai kwa wananchi hao kuangalia viwango na uhalisia  wa thamani ya ardhi wanapopeleka ombi lao kama kweli wanataka kupunguziwa.


Eneo hilo lenye Ukubwa wa ekari 118 liliingia kwenye Mgogoro Mwaka 2014 baada ya wananchi kuvamia Ardhi na kuweka Makazi ya kudumu jambo ambalo ililazimika kufikishwa mahakamani na hatimaye mwekezaji akashinda kesi na wananchi kushindwa hali ambayo imetoa Kiashiria cha kutafuta njia ya maridhiano nje ya mahakama.


Zaidi ya kaya 581 zimejiandisha kukusudia kulipia gharama za maeneo au Viwanja wanavyohodhi iwapo mwekezaji atawalegezea bei na kufikia shilingi 2500.

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KIBAHA TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • TANGAZO LA MNADA WA NG'OMBE KWA WAFANYA BIASHARA WA NYAMA NA NG'OMBE ,MTAA WA MTAKUJA KATA YA PANGANI, UNAOFANYIKA KILA ALHAMISI. March 13, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIBAHA MANISPAA YANG'ARA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 30, 2025
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • DKT.SHEMWELEKWA ATETA NA WAMILIKI WA VITUO VYA MAFUTA KIBAHA Na.Byarugaba Innocent, Kibaha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa amekutana na Wamiliki na Wafanyabiashara ya mafuta kuwakumbusha kuwa wazalendo kwa Taifa,kufa

    November 22, 2024
  • MHE.NDOMBA AZINDUA GARI MPYA AINA YA LANDCRUSER ILIYONUNULIWA KWA MAPATO YA NDANI

    November 21, 2024
  • Tazama Zote

Video

Mh. Waziri Mkuu akiwa ziarani Kibaha
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa