• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wananchi Manspaa ya Kibaha kunufaika na Huduma Bora, baada ya mji kupandishwa hadhi ya kuwa manspaa

Posted on: July 12th, 2025

Kibaha, Pwani – July 08, 2025


Serikali imetangaza rasmi kupandisha hadhi ya Halmashauri ya Mji wa Kibaha kuwa Manispaa ya Kibaha kuanzia tarehe 20 Juni 2025. Uamuzi huu ni sehemu ya mkakati wa serikali kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na kuharakisha maendeleo ya miji inayokua kwa kasi nchini.

Tangazo hilo limepokelewa kwa shangwe na matumaini makubwa na wakazi wa Kibaha, ambao sasa wanatazamia kunufaika na fursa mbalimbali zitakazotokana na hadhi hiyo mpya.

Akizungumza na wadau wa maendeleo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha Dkt Rogers Shemwelekwa amewata Wananchi na wadau wa maendeleo manspaa ya kibaha Kwa Tayari na kuendana na Kasi ya maendeleo ya Manspaa ili kujiletea maendeleo.

“Kupandishwa hadhi kwa Kibaha kuwa Manispaa ni ushahidi wa kazi kubwa iliyofanywa na wananchi na viongozi wao kwa pamoja. Tunakwenda kushuhudia maboresho ya miundombinu, huduma bora kwa wananchi, pamoja na ongezeko la ajira na fursa za kiuchumi.”

Amezitaja faida ya Halmashauri ya mji kupandishwa hadhi kuwa Manspaa ni

1. Miundombinu Bora:

Manispaa itapata bajeti kubwa zaidi kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa barabara, masoko, stendi za mabasi, mifereji ya maji, na taa za barabarani. Hii itarahisisha usafiri na biashara katika maeneo yote ya Kibaha.


2. Huduma Bora za Jamii:

Huduma za afya, elimu, na usafi wa mazingira zitaboreshwa. Shule na vituo vya afya vitapewa vifaa, watumishi na miundombinu ya kisasa ili kuhudumia wananchi kwa ufanisi zaidi.


3. Fursa za Ajira:

Miradi ya maendeleo na uwekezaji itakayotekelezwa italeta ajira kwa vijana na wanawake wa Kibaha, ikiwemo sekta ya ujenzi, biashara, na huduma.


4. Uwekezaji na Biashara:

Hadhi ya manispaa huvutia wawekezaji wa ndani na nje. Hii inamaanisha kujengwa kwa viwanda, maduka makubwa (supermarkets), hoteli, na huduma nyingine za kisasa zitakazoinua uchumi wa eneo hili.


5. Ushiriki wa Wananchi na Uwajibikaji:

Kwa kuwa Manispaa inakuwa na mifumo madhubuti ya usimamizi, wananchi watashirikishwa zaidi katika mipango ya maendeleo kupitia vikao vya kisheria na kamati za mtaa. Uwajibikaji wa viongozi utaimarika.


6. Kuongezeka kwa Mapato ya Ndani:

Kwa kuwa na vyanzo vingi vya mapato kama ushuru, tozo na ada halali, Manispaa itakuwa na uwezo mkubwa wa kugharamia miradi ya kijamii bila kutegemea sana misaada ya nje.


Mmoja wa wakazi wa Kibaha, Mzee Mfinanga (Njuweni), amesema:


“Kupandishwa hadhi ni kama tumepata mwanga mpya. Tunategemea kuona mabadiliko ya kweli, hasa barabara nzuri, huduma bora za afya na elimu kwa watoto wetu.”


Serikali imesisitiza kuwa hatua hii inakwenda sambamba na ajenda ya maendeleo kwa vitendo, na imetoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda na kuendeleza mafanikio haya.

Matangazo

  • INEC yahimiza Wananchi mikoa 16 kujitokeza uboreshaji Daftari awamu ya pili May 14, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Manspaa ya Kibaha kunufaika na Huduma Bora, baada ya mji kupandishwa hadhi ya kuwa manspaa

    July 12, 2025
  • Mkurugenzi Manspaa ya Kibaha Dkt Rogers Shemwelekwa awataka Wananchi kuchangamkia fursa za kibiashara Manspaa ya Kibaha

    July 10, 2025
  • WATENDAJI wa Kata Manspaa ya Kibaha watembelea Halmashauri ya Mji Tunduma

    July 09, 2025
  • Mh. Mchengerwa Aipongeza Sekondari ya Kibaha atoa Maagizo

    July 09, 2025
  • Tazama Zote

Video

Watendaji wa Kata Manspaa ya Kibaha waibua mazito mafunzo mbeya
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa