• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kibaha Town Council
Kibaha Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Usimamizi
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mazingira na Mipango Miji
      • UKIMWI
      • Maadili
      • Ustawi wa Jamii
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Viombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wazee 160 Mtaa wa Uyaoni waadhimisha siku ya wazee Duniani Kwa kupima Afya zao

Posted on: October 1st, 2025

Wazee 160 Uyaoni Waadhimisha Siku ya Wazee kwa Kupima Afya Kibaha


Kibaha, 01 Oktoba 2025 — Wazee 160 kutoka Mtaa wa Uyaoni, Kata ya Mailimoja, Manispaa ya Kibaha wameadhimisha Siku ya Wazee Duniani kwa kupima afya zao na kupata elimu juu ya lishe na magonjwa yasiyoambukiza.

Maadhimisho hayo yalifanyika tarehe 01 Oktoba 2025, yakilenga kuboresha afya na ustawi wa kundi hilo muhimu katika jamii.


Wataalamu wa afya kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha wametoa huduma mbalimbali ikiwemo upimaji wa hali ya lishe, kisukari, na shinikizo la damu. Aidha, wazee walipatiwa elimu ya lishe bora na namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza, hatua iliyolenga kuwawezesha kuishi maisha marefu yenye afya.


Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ni  Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon, ambaye aliwakilishwa na Afisa Tarafa ya Kibaha, Bi Catherine Njau. Akizungumza katika hafla hiyo, Bi Njau amewapongeza wazee kwa kujitokeza kwa wingi na kuadhimisha siku yao kwa njia ya kuhamasisha afya, mshikamano, na ushiriki katika shughuli za kijamii.


“Mmeonesha mfano wa kuigwa. Tunaomba mzidi kushirikiana na viongozi katika kuleta maendeleo kwa kutoa ushauri wa busara kutokana na uzoefu wenu mkubwa,” alisema.


Aidha, amehimiza viongozi wa kata na mitaa kuhakikisha wazee wanashirikishwa kikamilifu katika kamati mbalimbali, hasa kwa kuwa baadhi yao walikuwa watumishi katika sekta muhimu kama afya, ulinzi na maendeleo ya jamii, na wana uwezo wa kuchangia uboreshaji wa huduma na usalama.


Kwa upande wao, wazee wa Mtaa wa Uyaoni wameiomba serikali kuwawezesha kufikiwa na mikopo kutoka taasisi za kifedha, na mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri iwaguse wazee.


Pia wameiomba serikali iwajengee zahanati katika mtaa huo au kuwawekea kituo cha huduma ya kwanza, wakibainisha kuwa miongoni mwao wapo madaktari wastaafu ambao wanaweza kutoa huduma kwa urahisi kwa wenzao.


Mtendaji wa Mtaa wa Uyaoni, Bi Aminata Nombo, alithibitisha kuwa jumuiya hiyo ya wazee ina umoja wa watu 160 ambao wanashirikiana kwa karibu na kushikamana katika masuala ya kijamii.


Maadhimisho haya yameonesha umuhimu wa kuwatambua na kuwawezesha wazee kama sehemu muhimu ya maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO MWAKA -2050 July 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUND VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 02, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -MSAIDIZI KUMBUKUMBU II October 06, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Rc pwani aitaka Taasisi ya Elimu ya watu wazima kuleta matokeo chanya Sasa.

    October 02, 2025
  • Wazee 160 Mtaa wa Uyaoni waadhimisha siku ya wazee Duniani Kwa kupima Afya zao

    October 01, 2025
  • MRADI WA TACTIC MANISPAA YA KIBAHA KUONGEZA FURSA ZA UCHUMI KWA WANANCHI

    September 25, 2025
  • Wajasiliamali wadogo wanaopanga biashara zao pembeni mwa Barabara wamshukuru na kumpongeza Mkurugenzi Manispaa ya Kibaha

    September 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Matangazo Mubashara Hafla ya Utiaji Saini mikataba ya Soko la Mnarani na miundombinu ya Barabara
Picha za Kutembea

Kiungo cha Haraka

  • Sheria Ndogo(Ushuru wa magari ya abiria na mizigo)
  • Barua Pepe
  • Uujazi wa Viwanja
  • Muundo Wa Kiuongozi Halmashauri
  • Dira na Dhamira ya Halmashauri

Kiungo Kinachohusiana

  • Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Ofisi ya Raisi, Tawala za Serikali za Mikoa na Mitaa
  • Utumishi
  • Utumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani Ilipo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera za Siri
    • Disclamer
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Zote Zimahifadhiwa